YANGA HAITAFANYA DHARAU NA WACOMORO, LWANDAMINA ASISITIZA UMAKINI
YANGA HAITAFANYA DHARAU NA WACOMORO, LWANDAMINA ASISITIZA UMAKINI
Yanga imepangwa kuanza michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuwavaa Ngaya de Mbe ya Comoros.
Kocha wake, George Lwandamina amesema haitakuwa kazi rahisi na Yanga haitafanya mzaha hata kidogo.
"Michuano
ya Ligi ya Mabingwa Afrika ni mikubwa na migumu, inakutanisha mabingwa
wa nchi za Afrika. Hauwezi kuidharau timu yoyote," alisema.
Yanga ikifanikiwa kuwaondoa Wacomoro, itakutana na kati ya Zanaco ya Zambia au APR ya Rwanda ambazo ni timu ngumu.
Chini ya Lwandamina, Yanga imekuwa ikiendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
YANGA HAITAFANYA DHARAU NA WACOMORO, LWANDAMINA ASISITIZA UMAKINI
Reviewed by Unknown
on
2:03 PM
Rating:
No comments: