EXCLUSIVE: KAZI IPO, AZAM FC YASHUSHA KIPA WA TIMU YA TAIFA YA IVORY COAST, YUKO DAR

Uongozi
wa Azam FC umeamua hasa, baada ya kumshusha kipa kutoka Tenerife ya
Hispania, sasa kuna kipa wa timu ya taifa ya Ivory Coast.
Huyu ni Daniel Yeboah Tetchi ambaye yuko jijini Dar es Salaam tayari kumalizana na Azam FC ili aitumikie msimu ujao.
Kipa huyo mwenye umri wa miaka 31, alianza kuonyesha cheche zake akiwa Asec Mimosa ya Ivory Coast.
Pia amewahi kuitumikia Dijon ya Ufaransa katika kikosi chake cha pili.
Habari
za uhakika zinaeleza, Tetchi yuko katika nafasi kubwa ya kumalizana na
Azam FC lakini suala la kipa Mhispania linaweza kuweka ushindani mbele
yake.
EXCLUSIVE: KAZI IPO, AZAM FC YASHUSHA KIPA WA TIMU YA TAIFA YA IVORY COAST, YUKO DAR
Reviewed by Unknown
on
2:55 PM
Rating:

No comments: