Majibu ya Wakala wa Samatta kuhusu kujiunga na AS Roma






Dirisha la usajili kwa nchi nyingi hasa za Ulaya limeendelea kushika kasi kwa vilabu mbalimbali kuendelea kuongeza wachezaji wapya ama kupunguza kwa maana ya kuuza na kununua.

 Huku hapa Tanzania napo timu zikiendelea kujidhatiti kuliibuka taarifa ama fununu kuhusiana na mchezaji Mbwana Samatta anayechezea klabu ya Genk ya nchini Ubelgiji kutakiwa kujiunga na klabu ya As Roma ya nchini Italia inayoshiriki ligi kuu ya nchini humo yaani Serie A.
Taarifa ama fununu hizo zilionekana kuanzia kwenye mitandao ya kijamii yaani Twitter lakini baadae zikasambaa mpaka kufikia baadhi ya vyombo vya habari baadhi kuthitibisha taarifa hizo. Taarifa zilisema kuwa Samatta alitegemewa kupanda ndege kwenda kumalizana na As Roma baada ya kuwa klabu hizo mbili zimemalizana juu ya usajili wake.
www.shaffihdauda.co.tz ikaona ni vyema kujua undani wa taarifa hizi na kukufikishia mpenzi wa soka na ilimtafuta moja kwa moja wakala wa Mbwana Samata Nicholas Onise kutoa ukweli wa mambo ambaye alikataa kwa haraka tu na kuashiria kuwa hakuna mazungumzo yaliyokuwepo ama yaliyokuwa yamefanyika kumuhisha Samata kuelekea nchini Italia kama ilivyokuwa imeripotiwa awali. Onise amekanusha na kudai kuwa Samatta ni mchezaji wa Genk ana atacheza Genk.
Majibu ya Wakala wa Samatta kuhusu kujiunga na AS Roma Majibu ya Wakala wa Samatta kuhusu kujiunga na AS Roma Reviewed by Unknown on 2:46 PM Rating: 5

No comments:

Theme images by Colonel. Powered by Blogger.