MCHEZAJI WA TIMU YA MWANANYAMALA AANGUKA NA KUZIMIA UWANJANI, AKIMBIZWA HOSPITALI

SIKU ISMAIL ALIPOANGUKA UWANJANI NA KUPOTEZA MAISHA

Siku chache baada ya kinda wa Mbao FC timu ya vijana U 20 kuanguka uwanjani na kupoteza maisha, mchezaji mwingine ameanguka na kuzimia.

Katika hali isiyotarajiwa, beki wa timu ya Colombia FC ya Mwananyamala, Athumani Suwa, jana asubuhi alikata kauli baada ya kuzimia uwanjani kutokana na kugongana na mwenzake wakati wakiwania mpira kabla ya kukimbizwa katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar.


Tukio hilo lilitokea katika mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mwananyamala B, Dar.


Baada ya kufika hospitalini hapo na kushuhudia mchezaji huyo akiwa amewekwa katika chumba cha mapumziko baada ya kupatiwa huduma.


Akizungumza mmoja wa wachezaji wa timu hiyo ambaye alikuwepo katika mazoezi hayo, Ramadhan Ally, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo uwanjani.
MCHEZAJI WA TIMU YA MWANANYAMALA AANGUKA NA KUZIMIA UWANJANI, AKIMBIZWA HOSPITALI MCHEZAJI WA TIMU YA MWANANYAMALA AANGUKA NA KUZIMIA UWANJANI, AKIMBIZWA HOSPITALI Reviewed by Unknown on 5:45 AM Rating: 5

No comments:

Theme images by Colonel. Powered by Blogger.