TP MAZEMBE WAJIFUA TAIFA KWA UFICHO, WAZUIA MASHABIKI, WAANDISHI KUWAONA









Kikosi cha TP Mazembe wamejifua kwa nusu saa tu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo.

TP Mazembe kutoka DR Congo wako nchini kuwavaa Yanga katika mechi ya Kombe la Shirikisho, mechi itakayipigwa kesho kwenye uwanja huo.

Wachezaji wao walipoingia uwanjani hapo, walinzi walioongozana na kikosi hicho walianza kuzuia watu kuingia uwanjani hapo.

Walizuiwa watu mbalimbali wakiwemo waandishi na inaonekana Mazembe walijifua haraka na kwa muda mfupi na baada ya hapo walipanda basi na kurejea hotelini.
TP MAZEMBE WAJIFUA TAIFA KWA UFICHO, WAZUIA MASHABIKI, WAANDISHI KUWAONA TP MAZEMBE WAJIFUA TAIFA KWA UFICHO, WAZUIA MASHABIKI, WAANDISHI KUWAONA Reviewed by Unknown on 4:39 PM Rating: 5

No comments:

Theme images by Colonel. Powered by Blogger.